RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amekutana na kufanya mazungumzo na Sheikh Mohammed bin Rashid Al Makhtoum, ambapo viongozi hao walijadili nyanja mbalimbali za ushirikiano baina ya nchi hizo. Sheikh Mohammed ni makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu na mtawala wa Dubai, ambapo kiongozi huyo aliahidi na Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo biashara, uwekezaji na utalii. Katika maelezo yao viongozi hao walieleza azma ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu ambao ni wa kihistoria uliopo kati ya Zanzibar na Dubai. Kwa upande wake, Dk. Shein alimueleza kiongozi huyo juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Zanzibar katika kuhakikisha sekta ya utalii inaimarika sambamba na ongezeko la watalii wanaovitembelea visiwa vya zanzibar. Dk. Shein alisema ongezeko la wataalii kwa sasa wanavitembelea visiwa vya Zanzibar linaweza kuvuka watalii 500,000 kabla ya kufikia mwaka 2020. ...